• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MAWAKALA watakaojitoa ufahamu katika uchaguzi mkuu kukiona

Tarehe ya Kuwekwa: October 21st, 2020

 

 


Msimamiwa wa uchaguzi wa jimbo la Peramiho Simon Bulenganija ametoa onyo kwa mawakala wa vyama vya siasa watakaojitoa ufahamu kwa lengo la kuvuruga uchaguzi mkuu mkono wa sheria hautawaacha salama.

Bulenganija ametoa onyo hilo kwa nyakati tofauti wakati akiwaapisha kiapo cha kutunza siri mawakala wa vyama vya siasa ambao wameteuliwa na vyama katika Mji mdogo wa Peramiho na Kijiji cha Mpitimbi katika Jimbo la Peramiho Mkoani Ruvuma.

Amesema kwa wakala yeyeto atakayejito ufahamu kwalengo la kuvulruga uchaguzi mkuu, siku ya uchaguzi Oktoba 28, 2020 iwe,wakati wa kupiga kura, kuhesabu kura,kujumlisha kura na kutangaza matokea mkono wa sheria hauta muacha salama kwasababu zoezi la uchaguzi lipo kwamujibu wa kanuni taratibu na sheria za Nchi.

“Lazima mpime vizuri  kazi ya kusimamia maslahi ya chama   lakini pia  umuhimu na ulazima wa kuzingatia  sheria,kanuni,taratibu na maelekezo ya Tume”,alisema Bulenganija.

Amewataka mawakala kila wakala kutimiza jukumu alilopangiwa na kuacha kuingilia jukumu ambalo wakala hakupangiwa katika kipindi cha kupiga kura,kuhesabu kura  kujumlisha kura na kutangaza matokeo.  

Bulenganija ameongeza kwakusema vyama ambavyo havijawasilisha orodha ya majina ya mawakala wa vyama vyao katika Ofisi ya Msimamizi wa jimbo la Uchaguzi hawataruhiswa kusimamia uchaguzi  kwamujibu  wa maelekezo ya Tume,ambapo katika jimbo hilo vyama viwili tu ambavyo vimetimiza sharti hilo ambavyo ni Chama cha Maendeleo na Demokrasia (CHADEMA) na Chama cha Mapinduzi (CCM).


Amewakumbusha wanachi wote wenye sifa na vigezo kujitokeza kwa wingi kwenda katika vituo vyao walivyojiandikisha kwenda kupiga kura ifikapo siku ya jumatano Oktoba 28,2020 pasipo na shaka yoyote kwani Tumeya Uchaguzi imeimarisha ulinzi ili kuhakikisha kila mtu anapiga kura kwa uhuru. 

Amesema maandalizi yote ya zoezi la uchaguzi yanaenda vizuri na tayari Tume ya Taifa ya uchaguzi imeshafikisha vifaa kwa asilimia 98 ambavyo vinatakiwa katika kufanikisha zoezi hilo.

Kwaupande wake Msimamizi msaidizi wa Jimbo la uchaguzi Kangese Masanja amesema mawakala ni kundi la watu muhimu katika kufanikisha zoezi la uchaguzi ,hivyo nivema wakazingatia maelekezo yote yanayotolewa naTume na kujiepusha na udanganyifu wawapo katika vituo vya kupigia kura na kuwasiliana na msimsmizi mkuu wa kituo ambaye amepewa mamlaka na Tume ya kuwa mkuu wa kituo

Jimbo la Peramiho lina Kata 16,Vijiji 56,vituo vya kupigia kura 252 na jumla ya mawakala 509 waliapa kiapo cha kutunza siri nakutotoa siri  na kukiuka sheria ya kiapo adhabu yake ni kushughulikiwa na vyombo vya dola.

Ikumbukwe kwamba uchaguzi wa mwaka huu ni uchaguzi wa sita tangu Nchi ya Tanzania iingie kwenye mfumo wa vyama vingi mwaka 1992

Imeandikwa na

Jacquelen Clavery-Songea DC.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa