• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AZINDUA JENGO LA KUTOLEA HUDUMA YA KUSAFISHA FIGO PERAMIHO- ATOA WITO VIJANA KUACHA KUUZA FIGO

Tarehe ya Kuwekwa: July 21st, 2023


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ametoa wito kwa watanzania hususani vijana kujiepusha na kutoa figo zao kwaajili ya kufanya biashara ili kuepuka madhara makubwa yanayoweza kujitokeza.

Makamu wa Rais amesema hayo leo tarehe 21 Julai 2023 akiwa ziarani mkoani Ruvuma mara baada ya kuzindua Jengo la kutolea huduma ya usafishaji figo lililopo katika hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Joseph - Peramiho. Amesema tabia hiyo inaweza kuhatarisha Maisha ya mwanadamu hususani pale figo iliobaki inaposhindwa kufanya kazi.

Aidha Makamu wa Rais ametoa rai kwa watanzania kujenga tabia ya kupima afya walau mara moja kwa mwaka ili kuepukana na hatari za maradhi kufikia hatua mbaya zaidi. Makamu wa Rais amesema ni vema kuachana na ulaji usiofaa, unywaji wa pombe kupitiliza pamoja na kuhimiza kufanya mazoezi kuepukana na hali hiyo.

Halikadhalika Makamu wa Rais amewataka viongozi na watalaam wa afya kuendelea kutoa elimu ya namna ugonjwa huo unavyopatikana ili kuwasaidia wananchi kuepukana nao.

Makamu wa Rais amesema ugonjwa wa Figo ni miongoni mwa magonjwa yanayoongoza kusababisha vifo vya watu wengi duniani ambapo nchini Tanzania inakadiriwa kuwa kwa kila Watanzania mia moja Watanzania saba wanasumbuliwa na ugonjwa sugu wa figo. Ameeleza kwamba asilimia kumi (10) ya wagonjwa sugu wa figo nchini wamefikia hatua ya mwisho ambayo inahitaji matibabu mbadala ya figo, yaani kusafishwa damu au kupandikizwa figo nyingine.

Makamu wa Rais ameongeza kwamba serikali inatekeleza afua mbalimbali zenye lengo la kuzuia na kudhibiti ugonjwa wa figo na magonjwa mengine yasiyoambukiza ambapo hadi sasa zaidi ya Madaktari bobezi wa figo 20 na zaidi ya Wauguzi bobezi 10 wamehitimu mafunzo na wanatoa huduma kwenye hospitali mbalimbali. Amesema kufikia mwisho wa mwezi Juni, 2023, serikali imefanikiwa kutoa huduma za kusafisha damu kwa wagonjwa takribani 3,500, paamoja na kupandikiza figo kwa wagonjwa 74 katika Hospitali ya Taifa ya Muhimbili na wagonjwa 33 katika Hospitali ya Kanda ya Kati ya Benjamin Mkapa, Dodoma.

Dkt. Mpango amepongeza Hospitali ya Rufaa ya Mtakatifu Joseph – Peramiho kwa kutoa huduma ya kusafisha figo ambayo itakua msaada kwa wananchi wa mkoa huo na maeneo ya Jirani.

Kwa Upande wake Mbunge wa Jimbo la Peramiho na Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Sera Bunge na Uratibu Jenista Mhagama ameishukuru serikali kwa utekelezaji wa miradi mbalimbali ya maendeleo katika eneo hilo katika sekta za Afya, Elimu na Miundombinu.

Waziri Mhagama amesema zaidi ya shilingi milioni 400 zimetolewa kwaajili ujenzi wa stendi ya kisasa katika Halmashauri hiyo pamoja na ujenzi wa zahanati katika vijiji 50.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa