• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

MAKAMU wa Rais Dkt. Mpango afungua maonesho ya Nane nane 2023 Mkoani Mbeya

Tarehe ya Kuwekwa: August 2nd, 2023


Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amekemea tabia ya uvamizi na mtindo wa kubadili matumizi ya ardhi iliyotengwa mahususi kwa ajili ya Utafiti wa Kilimo.

Makamu wa Rais ametoa maagizo hayo leo tarehe 01 Agosti 2023 wakati akifungua maonesho ya Nane nane kitaifa yanayofanyika katika viwanja vya John Mwakangale mkoani Mbeya. Amesema maeneo mengi ya taasisi za utafiti yamevamiwa na kupimwa viwanja jambo ambalo linatishia utafiti wa kilimo na mifugo kwa kuwa vituo vya utafiti vitakosa maeneo ya kutosha ya kufanyia kazi.  

Makamu wa Rais amewataka watanzania kutambua kilimo ni sayansi na hivyo utafiti kilimo usipopewa kipaumbele basi mapinduzi ya kilimo yatabaki kuwa ndoto. Amesisitiza umuhimu wa kupima maeneo ya taasisi za utafiti wa kilimo, kupewa hati na kulindwa wakati wote. Vivyo hivyo ameelekeza mamlaka zinazohusika kutenga na kupima ardhi katika maeneo ya uzalishaji wa mbegu na kuyalinda dhidi ya uvamizi.

Vilevile Makamu wa Rais amekemea uwepo wa makundi makubwa ya mifugo yalioingizwa katika mikoa ya nyanda za juu kusini. Amesema madhara yake ni makubwa ikiwemo kuharibiwa sana kwa mazingira kuongezeka kwa migororo mingi kati ya wakulima na wafugaji, wanyama kama Tembo kukimbia bugudha ya mifugo na kuhamia kwenye makazi ya binadamu wakiharibu mazao na hata kuua watu. Amezitaka Wizara zote husika na Wakuu wa Mikoa kuchukua hatua thabiti kudhibiti uingizaji mifugo kinyemela katika maeneo yao ya utawala.

Makamu wa Rais ametoa wito kwa wakulima, wafugaji na wavuvi kuzingatia maelekezo ya wataalam ili kuweza kuzalisha pasipo kuathiri afya ya binadamu na mazingira kutokana na kuongezeka kwa matumizi yasiyo sahihi ya viuatilifu na kemikali nyingine jambo lenye athari kubwa kwa afya ya binadamu na viumbe hai vingine.

Ameongeza kwamba Serikali inaendelea kuimarisha miundombinu ya umwagiliaji nchini ikiwemo kujenga mabwawa ya kuvuna maji ya mvua kwa ajili ya umwagiliaji, ambapo lengo ni kufikia eneo la umwagiliaji la hekta 1,200,000 ifikapo mwaka 2025. Pia ametoa wito kwa wananchi kutumia na kutunza miundombinu hiyo ili iweze kutumika kwa muda mrefu na kusaidia kuleta tija.

Makamu wa Rais ametoa rai kwa wakulima kuongeza uzalishaji wa mazao ya chakula ili taifa liweze kujitosheleza kwa chakula na kupata fedha zaidi za kigeni kutokana na mazao mbalimbali. Amasema Serikali kwa upande wake itaendelea kuimarisha utoaji wa huduma za ugani kwa kuwapatia Maafisa Ugani vitendea kazi mbalimbali vikiwemo pikipiki, vifaa vya matibabu, uhimilishaji pamoja na vifaa vya kupima afya ya udongo.

Ameitaka Wizara ya Kilimo na Mifugo kuanza maandalizi ya kuchukua vijana wengine katika programu ya Jenga Kesho Iliyo Bora (Building a Better Tomorrow - BBT) pamoja na kuziagiza Wizara za Kilimo na Mifugo na Uvuvi kuona namna bora ya kushirikiana na Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa ili vijana wa JKT wanaojitolea wapewe kipaumbele kushiriki katika programu hiyo.

Makamu wa Rais ameendelea kusisitiza taasisi za fedha na mabenki hapa nchini kuendelea kushusha riba zaidi ili kuwasaidia wakulima na wafugaji. Ameitaka Wizara ya Kilimo na Fedha kufikiria kuanzishwa kwa  mfuko wa maendeleo ya kilimo utakaosaidia kushusha riba kwa wakulima, wafugaji na wavuvi.

Amewapongeza watafiti waliosaidia katika upatikanaji wa mbegu na kutoa wito kwa Wizara ya Kilimo kutafuta utaratibu wa kuwapa tuzo vijana na wabunifu wanaotoa suluhu ya mambo mbalimbali katika kilimo, ufugaji na uvuvi.

Kwa upande wake Waziri wa Kilimo Hussein Bashe amesema sekta ya kilimo inaendelea kuimarika kutokana na juhudi za serikali katika kuinua sekta hiyo ikiwemo kuongezeka kwa bajeti kufikia shilingi bilioni 970 kutoka bilioni 294. Ameongeza kwamba kuimarika kwa sekta hiyo kumepelekea kuzalishwa kwa kahawa tani 80000, tumbaku kilo milioni 120 huku uzalishaji wa pamba ukiongezeka mara mbili. Bashe ameishukuru serikali kwa kutoa shilingi bilioni 100 ili kusaidia makampuni ya pamba yaweze kununua zao hilo kwa wakulima.  

Waziri Bashe amesema maendeleo ya kilimo yanategemea ufanisi katika sekta zingine ikiwemo bandari. Ameongeza kwamba mabadiliko na uwekezaji wa tija katika bandari yanahitajika kwa sasa kwani yatasaidia wakulima katika kusafirisha mazao yao.

Pia amesema kuanzia mwaka 2024 nchi zote za Afrika zitapata mialiko ya kuhudhuria maonesho ya Nane nane huku akisisitiza mialiko hiyo haitahusisha viongozi pekee bali hadi wakulima na wanunuzi wa mazao wa nchi hizo. Ameongeza kwamba kufuatia kupanda hadhi kwa maonesho hayo kuwa ya kimataifa, juhudi mbalimbali zinaendelea ikiwemo kuboresha maeneo yanayotumika kwa ajili ya sherehe hizo kwa kuyajenga ili yawe ya kudumu.


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa