• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

KAMATI ya Siasa Wilaya ya Songea yatembelea miradi ya Maendeleo

Tarehe ya Kuwekwa: August 18th, 2023

KAMATI ya Siasa Wilaya ya Songea chini ya Mwenyekiti wake Mhe. Thomas Masolwa imetembelea miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa lengo la kujiridhisha na hatua za utekelezaji, viwango vya ubora pamoja na thamani ya fedha.

Akiwa katika ziara hiyo, Mhe. Masolwa amesema usimamizi na ufuatiliaji wa miradi ni muhimu sana hasa ikizingatiwa lengo la Serikali ni kuhakikisha inafikisha huduma kwa wananchi wake hivyo miradi isimamiwe ili iweze kukamilika mapema.

"Sisi kama Kamati ya siasa ya Wilaya, jukumu letu ni kuhakikisha miradi inatekelezwa kama maelekezo ya Serikali yanavyotolewa hivyo mafundi Viongozi hakikisheni miradi inakamilika kwa haraka na viwango vinavyokubaliwa na Serikali” amesisitiza Mhe. Masolwa.

Miradi iliyotembelewa ni pamoja na ujenzi wa madarasa 12 katika shule ya Sekondari Jenista Mhagama, mabweni 4 na vyoo matundu 20 unaogharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 834 kutoka Serikali Kuu, ujenzi wa shule ya msingi mpya ya Nambalapi inayogharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 331.1 kutoka Serikali kuu kupitia mradi wa BOOST na mwisho walitembelea shule ya Sekondari Maposeni ambapo kuna ujenzi wa madarasa 4, mabweni 2 na vyoo matundu 6 unaogharimu fedha kiasi cha shilingi milioni 362.2 kutoka katika kampuni ya Barrick Gold Mine.

Aidha, Mhe. Masolwa ameipongeza na kuishukuru Serikali ya Awamu ya Sita inayoongozwa na Mheshimiwa Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan na Mbunge wa Jimbo la Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama kwa kuendelea kuleta fedha za kuboresha miundombinu ya Elimu.

Vilevile Mheshimiwa Masolwa amewapongea Baraza la Madiwani, timu ya wataalamu ngazi ya Halmashauri, Kata na Vijiji pamoja na viongozi wote kwa usimamizi mzuri wa miradi.

Kwaupande wake Mwenyekiti wa Halmashauri Mheshimiwa Menas Komba amesema Halmashauri imejipanga vizuri katika kuisimamia miradi ili ikamilike kwa viwango vinavyokubaliwa ili Serikali iendelee kuleta fedha kwa ajili ya kutekeleza miradi mingine ya Maendeleo.

Nae Mkurugenzi  Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea Ndugu Neema Maghembe ametoa rai  kwa mafundi Viongozi kufanya kazi na waache tamaa ya kupokea miradi zaidi ya mmoja ili kuepuka kuchelewa kukamilika kwa miradi.

Ziara hiyo imehusisha Kamati ya siasa ya Wilaya, Mwenyekiti wa Halmashauri, Mkurugenzi Mtendaji na Wakuu wa Idara na Vitengo.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa