• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango Yakagua Miradi ya Maendeleo Songea Dc

Tarehe ya Kuwekwa: September 3rd, 2024



Kamati ya Fedha, Uongozi na Mipango (KFUM) ya Halmashauri ya Wilaya ya Songea, ikiongozwa na Mwenyekiti wake ambaye pia ni Mwenyekiti wa Halmashauri, Mhe. Menans Komba, imefanya ziara ya ukaguzi wa miradi mitano ya maendeleo leo, tarehe 3 Septemba 2024. Ziara hii ililenga kukagua utekelezaji na maendeleo ya miradi hiyo katika maeneo mbalimbali ndani ya halmashauri ya wilaya hiyo.


Kamati ilianza ziara yake kwa kukagua ghala la mazao lililopo katika Kata ya Mbinga Mhalule, Kijiji cha Matomondo. Ghala hili ni muhimu kwa ajili ya kuhifadhi mazao ya wakulima wa eneo hilo, lakini ujenzi wake umekwama kutokana na uhaba wa fedha. Kamati ilijadili makadirio ya fedha zinazohitajika kukamilisha ujenzi huo, ambapo Mwenyekiti alisisitiza umuhimu wa kuhakikisha rasilimali zinapatikana ili kukamilisha mradi huo haraka.


Kamati iliendelea na ziara kwa kukagua ujenzi wa matundu nane ya vyoo kwa wasichana katika Shule ya Msingi Matomondo. Mradi huo ulipokea shilingi milioni 14 kutoka Serikali Kuu. Hata hivyo, ujenzi umesimama ukisubiri kufunguliwa kwa bakaa. Pamoja na changamoto hizo, mradi uko katika hatua za mwisho za kukamilika.


Katika Kijiji cha Kizuka, kamati ilikagua mradi wa uboreshaji wa zahanati ya kijiji hicho, ambao ulipokea fedha katika mwaka wa fedha 2021/2022. Uboreshaji huo unalenga kuboresha chumba cha mama na mtoto, choo na bafu, pamoja na ujenzi wa matundu saba ya vyoo. Mradi huo umegharimu kiasi cha shilingi milioni 27.4, lakini bado haujakamilika. Mwenyekiti wa kamati, Mhe. Komba, alipendekeza tathmini ya gharama zinazohitajika ili kukamilisha ujenzi huo na tathimini ya gharama hizo ziwasilishwe siku ya majumuisho ili fedha zitolewe kukamilisha mradi huo.


Ziara hiyo pia ilijumuisha ukaguzi wa ujenzi wa matundu 13 ya vyoo, kitakasa mikono, pamoja na mnara wa tenki la maji katika Shule ya Msingi Jenista. Aidha, kamati ilikagua Zahanati ya Mipeta ambapo miradi hiyo yote ipo katika hatua za ukamilishaji.


Mwenyekiti wa Kamati, Mhe. Menans Komba, amewataka watumishi wanaosimamia miradi hii kuwa waaminifu na wenye uadilifu katika usimamizi wa miradi ya serikali. Aliongeza kuwa ucheleweshaji wa kukamilika kwa miradi hiyo unachelewesha maendeleo kwa jamii, hivyo ni muhimu kuharakisha utekelezaji wake ili kuboresha maisha ya wananchi wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • MAFUNZO YA UBORESHAJI WA DAFTARI LA KUDUMU LA WAPIGA KULA YAMEANZA SONGEA DC

    April 29, 2025
  • MHE . JENISTA MHAGAMA AZINDUA MADARASA 27 NA VYOO MATUNDU 44, SONGEA DC

    March 16, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa