• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAPONGEZWA KWA KUPATA HATI SAFI KWA MWAKA WA FEDHA 2023/2025

Tarehe ya Kuwekwa: June 18th, 2025


Katibu Tawala wa Mkoa wa Ruvuma, Bi Marry Makondo, akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa kupata hati safi katika ukaguzi wa Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali (CAG) kwa mwaka wa fedha 2023/2024.

Bi Makondo alitoa pongezi hizo leo Juni 18, 2025 wakati wa Mkutano maalum wa Baraza la Madiwani uliofanyika katika ukumbi wa Halmashauri ambapo alisoma hotuba kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa. Alimpongeza Mwenyekiti wa Halmashauri, madiwani wote, pamoja na kumtambua Mbunge wa Jimbo la Peramiho kwa mchango wake katika kufanikisha hati hiyo safi.

"Hati hii safi imepatikana kutokana na juhudi zenu za pamoja katika kujibu na kutetea hoja za Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali," alisema Bi Makondo.

Katika mkutano huo, ilielezwa kuwa kati ya hoja 32 zilizotolewa na Mkaguzi Mkuu, hoja 18 tayari zimefungwa, hoja 14 zipo katika hatua za utekelezaji, na hoja 7 kutoka miaka ya nyuma bado hazijatekelezwa kikamilifu.

Katika hatua nyingine, Bi Makondo aliwapongeza wataalamu wa Halmashauri kwa uwajibikaji mzuri na kuwapatia vyeti vya pongezi watumishi waliofanya vizuri. Watumishi waliotunukiwa vyeti ni Hadija Boffu (Mweka Hazina), Ignus Kong’oa (Mkaguzi wa Ndani), Nurdin Seleman na Lameck Joshua (Wahasibu). Alisema kuwa vyeti hivyo vitachochea ari ya utendaji bora kazini.

Akiwasilisha taarifa ya hoja za CAG kwa mwaka 2023/2024, Mkaguzi wa Ndani wa Halmashauri, Bw. Ignus Kongowa, alieleza kuwa Halmashauri ya Wilaya ya Songea imeendelea kufanya vizuri ambapo imepata hati safi kwa miaka mitatu mfululizo: 2021/2022, 2022/2023, na sasa 2023/2024, jambo linaloonyesha juhudi kubwa katika kujibu hoja za ukaguzi.

Kwa upande wake, Makamu Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Mhe. Simon Kapinga, akizungumza kwa niaba ya Mwenyekiti wa Halmashauri, alitoa shukrani kwa kamati zote za madiwani kwa juhudi zao zilizowezesha Halmashauri kupata hati hiyo safi. Aidha, alimhakikishia Mkaguzi wa Nje kuwa hoja zilizobaki zitafanyiwa kazi ipasavyo ili Halmashauri iendelee kupata hati safi kwa miaka ijayo.

Naye Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, kwa niaba ya timu nzima ya watendaji, aliwashukuru wote waliochangia mafanikio hayo. Aliahidi kuendelea kutoa ushirikiano kwa Mkaguzi wa Nje katika kuhakikisha hoja zote zinazobakia zinafutwa, sambamba na kuwashukuru Waheshimiwa Madiwani kwa ushirikiano mkubwa waliompatia katika kipindi chao cha uongozi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • VIKUNDI 28 VAPATIWA MIKOPO YA TSH MILIONI 249 NA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    July 03, 2025
  • ZAIDI YA MILIONI 600 ZIMETUMIKA KUJENGA STEND YA KISASA PERAMIHO

    July 01, 2025
  • Ujenzi wa Mradi wa Barabara Likuyufusi–Mkenda ni fursa mpya ya Maendeleo ya Songea Dc.

    June 20, 2025
  • WASIMAMIZI WA MIRADI WASISITIZWA KUZINGATIA UADILIFU NA UFANISI KATIKA USIMAMIZI WA MIRADI YA MAENDELEO SONGEA DC

    June 19, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa