• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YANG’ARA MAONESHO YA NANENANE, KIMKOA

Tarehe ya Kuwekwa: August 11th, 2025


Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi Elizabeth Mathias Gumbo, amewapongeza Wataalamu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi kwa kufanya vyema na kushika nafasi ya pili, kati ya halmashauri nane zilizopo mkoa wa Ruvuma, katika Maonesho ya Nanenane ambayo Kimkoa yalifanyika Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga.

Akizungumza mara baada ya kupokea cheti hicho, Bi Elizabeth aliwashukuru watumishi wa idara ya kilimo, mifugo na uvuvi kwa kuiwakilisha vyema Halmashauri, akibainisha kuwa mafanikio hayo yametokana na mshikamano wa timu nzima kutoka Idara ya hiyo.

“Natumia fursa hii kuwapongeza idara ya kilimo kwa kufanya vizuri katika maonesho haya, Hii inaonesha mshikamano mlionao ndio umesababisha kufanya vizuri katika maonesho haya. Niwaombe taaluma mliyoionesha kwenye maonesho hayo muihamishie kwa wakulima wetu ili kuongeza tija katika kilimo, hususani tunapoelekea msimu mpya wa kilimo,” alisema Bi Elizabeth Gumbo

Kwa upande wake, Kaimu Mkuu wa Idara ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi, Ndugu Godson Msalilwa, alisema siri ya ushindi huo ni mshikamano na ushirikiano wa karibu baina ya wataalamu wote wa idara hiyo.

Alifafanua kuwa maonesho hayo, yaliyofanyika katika Viwanja vya Amani Makolo, Halmashauri ya Wilaya ya Mbinga, yalitoa nafasi kwa Halmashauri ya Songea kuonesha teknolojia mbalimbali ikiwemo uzalishaji wa mazao ya bustani, ufugaji wa sungura na kuku, pamoja na usindikaji wa mazao ya mihogo kwa vikundi vya usindikaji.

Maonesho ya Nanenane hufanyika kila mwaka kwa lengo la kutoa elimu, kuonesha ubunifu na kuhamasisha maendeleo ya sekta ya kilimo, mifugo na uvuvi nchini ambapo maonesho ya mwaka huu 2025 yamebeba kauli mbiu isemayo "Chagua Viongozi Bora kwa Maendeleo Endelevu ya Kilimo Mifugo na Uvuvi 2025”

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa