• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAENDESHA MAFUNZO YA UONGEZAJI VIRUTUBISHO KWENYE CHAKULA

Tarehe ya Kuwekwa: September 29th, 2025


Halmashauri ya Wilaya ya Songea kupitia Idara ya Afya, leo Septemba 29, 2025 imeendesha mafunzo ya uongezaji virutubisho kwenye chakula kwa ajili ya kuboresha lishe na afya za wananchi. 

Mafunzo hayo yalifunguliwa na Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya hiyo, Dkt. Scholastica Mapunda.

Akizungumza katika ufunguzi huo, Dkt. Mapunda alisisitiza umuhimu wa matumizi ya virutubishi kupitia mashine za kusaga nafaka, akieleza kuwa serikali kwa kushirikiana na Wizara ya Afya imejipanga kuhakikisha lishe bora inapatikana kwa wananchi wote ili kupunguza tatizo la udumavu na maradhi yanayotokana na lishe duni.


Aidha, alitoa wito kwa watendaji kusimamia sheria na kanuni zitakazohakikisha mashine mpya za kusaga nafaka zinazoongeza virutubishi zinafanya kazi ipasavyo, ili unga utakaopatikana uwe na viwango vya afya vinavyohitajika.



Kwa upande wake, Afisa Lishe wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Joyce Sipira, aliainisha aina za virutubishi vinavyoongezwa kwenye chakula ikiwemo zinki, folic acid, madini chuma na vitamin B12. Alieleza kuwa upungufu wa virutubisho hivyo unaweza kusababisha matatizo ya kiafya kama vile mgongo wazi, kichwa kikubwa na mdomo sungura kwa watoto, pamoja na utapiamlo kwa watu wazima.


Bi. Sipira pia aliwataka watendaji kuwa mabalozi wa elimu hiyo kwa wananchi, kwa kuondoa dhana potofu zinazohusiana na matumizi ya virutubishi.



Washiriki wa mafunzo hayo nao walipata nafasi ya kutoa shukrani, ambapo kwa niaba ya wasindikaji wa nafaka, Bw. Betodi Joseph alisema, “Tunashukuru sana kwa mafunzo haya, kwani kupitia mitambo hii mipya tunatarajia jamii yetu itapata unga wenye ubora na hivyo kuwa na afya bora.”


Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa