• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA YAADHIMISHA SIKU YA LISHE KITAIFA KWA KUHAMASISHA LISHE BORA

Tarehe ya Kuwekwa: October 30th, 2024


Halmashauri ya Wilaya ya Songea imeadhimisha Siku ya Lishe Kitaifa katika Kata ya Mpitimbi, ikitoa wito kwa wananchi kuzingatia lishe bora kama msingi wa afya na maendeleo ya jamii.


Kaimu Mganga Mkuu wa Halmashauri hiyo, ndugu Evaristo Ngalowaka, aliongoza maadhimisho hayo kwa kusisitiza umuhimu wa kuwekeza katika vyakula vyenye virutubisho sahihi ili kujenga jamii yenye afya bora na nguvu kazi imara.


Maadhimisho haya yaliakisi dhamira ya Halmashauri ya kuhakikisha kuwa kila mwananchi anapata elimu na uelewa wa kutosha juu ya umuhimu wa lishe bora. Katika hotuba yake, ndugu Evaristo aliipongeza Halmashauri kwa juhudi zake za kuimarisha afya ya jamii kwa kutoa elimu ya lishe hadi maeneo ya pembezoni.


Alieleza kuwa mpango huu wa elimu unaendeshwa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa afya na maendeleo, ikiwa ni moja ya mikakati ya Halmashauri kuzuia magonjwa yasiyo ya kuambukiza kama kisukari na shinikizo la damu, ambayo yanachochewa na utumiaji wa vyakula vyenye mafuta na sukari nyingi.


“Tunajivunia kuona Halmashauri yetu inachukua hatua madhubuti za kutoa elimu ya lishe bora kwa wananchi wetu wote, hasa vijijini ambako uelewa kuhusu lishe bado ni changamoto. Tunataka kuhakikisha kuwa kila mwananchi anajua umuhimu wa lishe bora kwa afya ya mwili na maendeleo ya kiuchumi,” alisema ndugu Evaristo


Aidha, ndugu Evaristo alisisitiza kuwa lishe bora ina mchango mkubwa katika kuimarisha nguvu kazi ya taifa na kupunguza gharama za matibabu. Aliitaja jamii yenye afya bora kuwa ndiyo msingi wa maendeleo ya taifa.


Kwa kuhitimisha, ndugu Evaristo aliwasihi wananchi kuwa mabalozi wa lishe bora katika jamii zao. Alisema, “Halmashauri yetu itaendelea kusimama na nyinyi ili kufanikisha malengo ya kuwa na jamii yenye afya njema. Tunawaomba nanyi mshiriki nasi kwa kutoa elimu kwa familia na majirani zenu ili vizazi vijavyo vipate afya bora na nguvu kazi yetu iweze kuchangia kikamilifu katika maendeleo ya nchi yetu.” Maadhimisho haya yamebeba kauli mbiu isemayo "Mchongo ni Afya Yako Zingatia Unacho Kula"

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa