• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

HALMASHAURI ya Songea yagawa pembejeo bure kwa wakulima wa ufuta

Tarehe ya Kuwekwa: December 3rd, 2020

HALMASHAURI ya Wilaya ya Songea yagawa pembejeo bure kwa wakulima wa zao la ufuta

Halmashauri ya wilaya ya Songea Mkoani Ruvuma imegawa mbegu ya ufuta bure kwa wakulima wa zao la ufuta katika Kata ambazo zinazalisha zao hilo kwa wingi kwa msimu wa kilimo wa mwaka 2020 /2021.

Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashuri hiyo Bw Simon Bulenganija amesema ametumia kiasi cha sh. milioni 10 kwa ajili ya kununua mbegu hiyo kwa lengo la kuwasaidia wakulima ili waweze kuongeza uzalishaji kutoka gunia tatu hadi tano kwa ekari moja,tofauti na awali wakulima walikuwa wakizalisha gunia moja hadi tatu kwa ekari moja kwakutuia mbegu ya kienyeji.

Ametaja idadi ya kilo zilizonunuliwa na kusambazwa kwa wakulima kuwa ni kilo 1000 na aina ya mbegu ni Lindi  02 zilizonunuliwa kutoka Kituo cha Utafiti wa Mazao cha Naliendele  kilichopo  Mkoani Mtwara.

Amezitaja kata na idadi ya kilo zilizosambazwa kuwa ni kata Muhukuru Barabarani na Lilahi ambao wamepata kilo 225,Kata ya Matimira  kilo 180,Kilagano kilo 180,Kizuka 180,Ndongosi kilo 90  na Magagura kilo 90.

Bulenganija ameyataja malengo ya kusambambaza mbegu hiyo ni  kuwapunguzia wakulima gharama ya kununua mbegu ya ufuta ambayo huuzwa shilingi 10,000 kwa kilo moja pia kuongeza uzalishaji na Serikali iweze kupata mapato kupitia ushuru unaotolewa na wakulima mara baada ya kuuza kupitia vyama vyao vya ushirika.

Kwa upande wake Afisa Kilimo Mazao wa Halmashauri hiyo Norbert Rugonza amewashauri  wakulima wa zao la ufuta wasitegemee matokeo chanya kwenye  kilimo bila kusimamia vizuri na  kufuatilia wakati wa uzalishaji.

Amesema wakulima ambao wamebahatika kupata mbegu hizo wanatakiwa kuzitumia kama shamba darasa kwakuzalisha kwa wingi na kusambaza kwa wakulima wengine kwenye msimu wa kilimo wa mwaka 2021 /2022.  

Amesema mbegu ya aina ya lindi 02 ni mbegu bora na nzuri kwa kilimo cha ufuta kwa sababu ni mbegu ambayo inastahimili magonjwa hivyo ni vema wakulima wakaachana na dhana potofu ya kwamba mbegu za kisasa zina matatizo ya kushambuliwa na magojwa na wadudu jambo ambalo halina ukweli.

Kwa upande wake Afisa Ushirika wa  Halmashauri ya Wilaya ya Songea Shekiel Masawe amesema katika msimu wa mwaka 2018/2019 ilifanikiwa kuzalisha zao la ufuta kilo milioni 1,316,227 na katika msimu wa kilimo wa mwaka 2019/2020 ilizalisha zao la ufuta kilo milioni 2,378,172 na kufanikiwa kuingiza mapato ya Zaidi ya shilingi milioni 400.

Imeandaliwa na

Jacquelen clavery

Songea DC

 

 

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa