• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

DC NDILE AIPONGEZA HALMASHAURI KWA USIMAMIZI BORA WA MIKOPO YA ASILIMIA 10

Tarehe ya Kuwekwa: August 1st, 2025

Mkuu wa Wilaya ya Songea, Mhe. Kapenjama Ndile, ameipongeza Halmashauri ya Wilaya ya Songea kwa usimamizi mzuri na uadilifu katika utoaji wa mikopo ya asilimia 10 kwa vikundi vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu, kama ilivyoelekezwa na Serikali.

Akizungumza wakati wa hafla ya utoaji wa mikopo hiyo iliyofanyika katika ukumbi wa Jenista Mhagama uliopo Shule ya Sekondari Maposeni, Mhe. Ndile alisema amefurahishwa na namna Halmashauri ya Wilaya ya Songea inavyotekeleza agizo la Serikali kwa ufanisi mkubwa chini ya uongozi wa Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri, Bi. Elizabeth Gumbo.


“Tunapokuwa na watendaji makini wanaojua wajibu wao na wanaojali wananchi, utekelezaji wa mipango ya Serikali huwa rahisi hongera sana Mkurugenzi na timu yako kwa kusimamia vema mchakato huu muhimu kwa maendeleo ya jamii yetu,” alisema Mhe. Ndile.


Aidha, Mkuu huyo wa Wilaya alisisitiza umuhimu wa vikundi vinavyonufaika na mikopo hiyo kuhakikisha wanazitumia kwa malengo yaliyokusudiwa na kuzirudisha kwa wakati, ili kutoa nafasi kwa vikundi vingine kufaidika.


“Fedha ina uwezo wa kubadili maisha ya mtu, lakini pia inaweza kukupotosha iwapo hutakuwa makini, nawasihi muwe waangalifu msije mkatumia fedha hizi kwa matumizi yasiyo ya lazima na mkasahau malengo yenu,” aliongeza.


Awali, akifungua hafla hiyo, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Songea, Bi. Elizabeth Gumbo, alisema kuwa zoezi hilo ni muendelezo wa utoaji wa mikopo ya asilimia 10 ya mapato ya ndani ya Halmashauri ambapo zaidi ya shilingi milioni 247 zimetolewa kwa vikundi 28 vya wanawake, vijana na watu wenye ulemavu.


Kwa upande wao, wanufaika wa mikopo hiyo walieleza furaha yao na kuishukuru Halmashauri kwa fursa waliyoipata. Akizungumza kwa niaba ya wenzake, Stumai Willo alisema mikopo hiyo itawasaidia kukuza mitaji ya shughuli zao za kiuchumi na kupunguza utegemezi katika familia.


“Tunashukuru sana Halmashauri kwa kutuamini na kutuwezesha. Pia tunamshukuru Mbunge wetu Mhe. Jenista Mhagama na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuona umuhimu wa makundi maalum,” alisema Stumai.


Mikopo hiyo ni utekelezaji wa agizo la Serikali linalozitaka Halmashauri kutenga asilimia 10 ya mapato ya ndani kwa ajili ya kuwawezesha wanawake, vijana na watu wenye ulemavu kiuchumi.

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • STENDI MPYA NA YA KISASA YA PARANGU, YAANZA KUONESHA NURU

    October 23, 2025
  • WATAHINIWA 5157 WA DARASA LA NNE SONGEA DC, WAANZA MITIHANI YAO LEO

    October 22, 2025
  • MKURUGENZI WA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA AWASISITIZA WANANCHI / WATUMISHI KUJITOKEZA KUPIGA KURA OKTOBA 29, 2025

    October 21, 2025
  • SERIKALI YAIMARISHA HUDUMA ZA AFYA SONGEA DC: ZAIDI YA MILIONI 891 ZATOLEWA KUJENGA VITUO VIPYA VYA AFYA

    October 18, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa