• Malalamiko |
    • Wasiliana nasi |
    • Maswali ya mara kwa mara |
    • Barua pepe za watumishi |
Songea District Council
Songea District Council

Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Halmashauri ya Wilaya ya Songea

  • Mwanzo
  • Kuhusu sisi
    • Historia
    • Dira na Dhima
    • Muundo wa Uongozi
  • Huduma
    • Huduma za Elimu
    • Huduma za Afya
    • Huduma za Maji
  • Utawala
    • Eneo la Utawala
    • Braza la Madiwani
    • Idara
      • Utumishi na Utawala
        • Maliasili
      • Mipango, Takwimu na Ufuatiliaji
      • Fedha na Biashara
      • Maendeleo ya Jamii
      • Kilimo na Umwagiliaji
      • Mifugo na Uvuvi
      • Elimu Msingi
      • Elimu Sekondari
      • Afya
      • Ujenzi na Zimamoto
      • Mawasiliano Serikalini
      • Ardhi
      • Fedha na Uhasibu
    • Vitengo
      • Internal Auditor
      • TEHAMA
      • TASAF
      • Ugavi na Manunuzi
      • Usafi Mazingira na Taka ngumu
      • Mawasiliano Serikalini
      • Maendeleo ya Miundombinu Mjini na Vijijini
      • Mawasiliano Serikalini
      • Sheria
  • Machapisho
    • Miongozo
    • Taratibu
    • Ripoti
    • Sheria
    • Fomu za Maombi
  • Kituo cha habari
    • Taarifa kwa vyombo vya Habari
    • Video
    • Hotuba
    • Albam ya Picha
    • Habari
    • Matukio
  • Miradi
    • Miradi iliyokamilika
    • Miradi ya Afya
    • Boost
    • Swash
  • Madiwani
  • Tarafa
  • Fursa za Uwekezaji
  • Shule
    • Shule za Msingi
    • Shule za Sekondari

ASILIMIA 60 ya magonjwa anayo ugua binadamu yanasababishwa na wanyama

Tarehe ya Kuwekwa: October 5th, 2020

MTAALAM kutoka Wizara ya Mifugo na Uvuvi Dr. Justine Assenga  amesema  zaidi ya asilimia 60 ya magonjwa anayougua binadamu yanasababishwa na wanyama.

Dr.Assenga ameyasema hayo kwenye mafunzo ya utayari wa kukabili magonjwa ambukizi kwa timu za dharura za kukabili magonjwa kutoka mikoa hatarishi ya Ruvuma na Mtwara ambayo yanafanyika kwa siku tano kwenye ukumbi wa Hoteli ya Tiffany mjini Mtwara.

Kwa mujibu wa Mtaalam huyo kati ya asilimia hizo,asilimia 75 ya magonjwa hayo yanaambukizwa na wanyamapori na asilimia 20 kutoka wanyama wanaofugwa.

Ameyataja magonjwa sita hatarishi  ya milipuko kuwa ni kimeta,kichaa mbwa,bonde la ufa,mafua makali ya ndege,kutupa mimba na ebola na amewataja baadhi ya wanyama ambao ni hatarishi katika kusambaza magonjwa hayo kuwa ni popo na panya.

Akifungua mafunzo hayo,Mkurugenzi wa  Maafa kutoka Ofisi ya Waziri Mkuu Kanali  Jimmy Matamwe ameitaja dhana ya afya moja kuwa inawakutanisha wataalam na wadau kutoka sekta mbalimbali hususani sekta ya afya,mazingira,maliasili,mifugo na wanahabari kutekeleza agenda ya usalama wa afya duniani.

“Dhana ya afya moja inatumika zaidi kwa kuzingatia kuwa vimelea vingi vinavyosababisha magonjwa ya binadamu,asilimia 60 vinatoka kwa wanyamapori na mifugo,maambukizi yanatokea pale binadamu anapoingilia masikani ya wanyama hao bila tahadhari”,alisema.

Hata hivyo amesema kwa nchi za Afrika hali ni hatarishi zaidi kwa kuzingatia kuwa bara hili hususani sehemu ambazo zinakaribia mapori makubwa ya wanyama ikiwemo Kongo Basin ni kitovu cha magonjwa ya milipuko kama vile ebola na homa ya bonde la ufa na hivi sasa ni virusi vya corona.

Kanali Matamwe amesema imedhirika kuwa ushirikiano wa watalaam katika mifumo ya afya moja  hivi sasa ni agenda ya dunia nzima kwa sababu inapunguza gharama katika kushughulikia tishio la magonjwa yanayotokana na vimelea vyenye uwezo wa kutoka kwa wanyama kwenda binadamu.

Amesema Tanzania sio kisiwa hivyo kutokana na ongezeko la watu duniani,mabadiliko ya tabianchi na utandawazi umekuwa na mwingiliano mkubwa baina ya watu na wanyama katika mazingira yao na kusababisha kueneo kwa vimelea kwa haraka zaidi na kusababisha magonjwa kwa binadamu,wanyama na mimea.

Kwa upande wake Mwakilishi wa Shirika la Chakula Duniani (FAO) Niwael Mtui ameyataja malengo ya kutoa mafunzo kwa timu ya afya moja ni  kuwajengea uwezo washiriki ili waweze kuzuia na kukabiliana na magonjwa ya mlipuko kabla hayajatokea.

Mafunzo ya utayari wa kukabili magonjwa ambukizi ya mlipuko kwa timu za dharura yanafadhiliwa na FAO kwa kushirikiana na Ofisi ya Waziri Mkuu ambayo yalianza kutolewa mwaka 2018.

Imeandikwa na Jacquelen Clavery

Oktoba 5,2020

Matangazo

  • Tangazo la Kuitwa kwenye Usaili Julai 2022 June 22, 2022
  • TANGAZO LA FURSA ZA KAZI KATIKA SHIRIKA LA UMOJA WA MATAIFA LA KUHUDUMIA WAKIMBIZI (UNHCR) August 26, 2022
  • TANGAZO LA KAZI October 13, 2022
  • WANAFUNZI WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA 2021. December 18, 2020
  • Ona Zote

Habari Mpya

  • KIKAO CHA MAAFISA HABARI KIMEMALIZIKA KWA KUWEKA MAKUBALIANO ENDELEVU KWA MASLAHI MAPANA YA NCHI

    May 24, 2025
  • MADAKTARI BINGWA WA DKT. SAMIA, WANATEGEMEA KUTOA HUDUMA ZA KIBINGWA NA UBINGWA BOBEZI KATIKA HOSPITALI YA HALMASHAURI SONGEA

    May 21, 2025
  • MKIMBIZA MBIO ZA MWENGE KITAIFA, AIPONGEZA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    May 11, 2025
  • BARAZA LA MADIWANI SONGEA DC, LIMEMSHUKURU MHE. RAIS NA WAZIRI WA AFYA KWA KUIHESHIMISHA HALMASHAURI YA WILAYA YA SONGEA

    April 29, 2025
  • Ona Zote

Video

NGOMA YA LIZOMBE
Video Zaidi

Kurasa za Karibu

  • Tovuti ya Mkoa wa Ruvuma
  • Tovuti ya Manispaa ya Songea
  • Tovuti ya Halmashauri ya Mji Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Mbinga
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Namtumbo
  • Tovuti ya Halmashauri ya Wilaya Tunduru
  • Tovuti ya Halmashauri ya Madaba
  • Tovuti ya Halmashauri ya Nyasa

Tovuti Muhimu

  • Utumishi wa umma
  • Baraza la mitihani la Taifa
  • National Website
  • Tamisemi
  • Sekretarieti ya ajira
  • Tovuti kuu ya serikali

World visitors tracker

world map hits counter

Idadi ya Watembeleaji

free HitCounter

Ramani ya Maeneo

Wasiliana nasi

    Halmashauri ya Wilaya Songea

    Anuani ya Posta: P.o.box 995, Songea

    Simu: 2602320 / 2602176

    Simu ya mkononi:

    Barua pepe: dedsongea@songeadc.go.tz

Mawasiliano Mengine

   

    • Sera ya Faragha
    • Kanusho
    • Maswali ya mara kwa mara
    • Ramani Tovuti
    • Huduma

Copyright ©2017 songeadc.go.tz. Haki imehifadhiwa